Utafiti mpya uliofanywa na watafiti wa Chuo Kikuu cha Berkeley nchini Marekani na kuchapishwa katika jarida la Proceedings of the National Academy of Sciences unaonyesha kwamba matajiri wengi wanaongozwa na kutawaliwa na tama na wana uwezekano mkubwa zaidi wa:
(1) Kudanganya ili kujishindia zawadi au bahati nasibu
(2) Kuiba pipi kutoka kwa watoto
(3) Kutorudisha chenji iliyozidi
(4) Kutofuata sheria za barabarani
Watafiti hawa wanaonya kwamba matokeo ya utafiti huu yasichukuliwe kama chanzo cha kuwachukia matajiri bali yachukuliwe kama changamoto ya kupunguza pengo kati ya matajiri na masikini.
Sijui kama matajiri wetu nao wana tabia kama hizi za wenzao wa Marekani. Habari zaidi kuhusu utafiti huu zinapatikana HAPA
Sijui kama matajiri wetu nao wana tabia kama hizi za wenzao wa Marekani. Habari zaidi kuhusu utafiti huu zinapatikana HAPA

No comments:
Post a Comment